ZA UKWELI SANA

HII NDIO TOFAUTI KATI YA DADY/MAMY AND FATHER/MOTHER

mamy na dady family.

 Haya ni maneno yaliyozoeleka sana kwenye matumizi ya kawaida ya kila siku ya familia zetu,na baadhi ya familia tumekuwa tukiyatumia bila kufahamu usahihi wake kwamba ni sehemu gani au mahala gani maneno haya yanayoelekea kuwa na maana moja lakini kiuhalisia sio kweli kwamba yana maana moja ya kimantiki labda kimuundo tu.
 Neno Dady/mamy hili hutumika miongoni mwa jamii chache sana barani africa,maneno haya humaanisha mzazi wa kike au wa kiume,lakini pia father/mother humaanisha mzazi wa kike na wa kiume miongoni mwa jamii nyingi sana sana za ki africa,japo yanatumika kuleta maana moja lakini yana utofauti mkubwa sana kimaana kama ifuatavyo;
   
  neno mamy/dady haya ni majina ya wazazi wengi waliojiandaa vizuri kutunza na kulea familia zao,mara nyingi watoto katika familia hizi huwa ni wachache na waliozaliwa kimpangilio maalumu,wazazi katika familia hizi huwa ni marafiki sana na watoto,watoto huwapenda sana haswa mzazi wa kiume,husomeshwa katika shule nzuri,hupatiwa mavazi mazuri sana,nyumba za familia hizi hutengewa maeneo mazuri kwa ajili ya michezo,na huwa na vifaa kwa ajili ya kuwaweka sawa kimwili na kiakili pia kama vitenesi,mipira,computer games na wakati mwingine nyumba huwekewa maeneo ya kuogelea maarufu kama swimming pool,katika familia hizi watoto mara zote huwa wasafi kubadilisha vyakula na vinywaji huwa ni jambo la kawaida sana,wakati mwingine pia husaza,mavazi mafupi kwa watoto   
wa kike huwa si dhambi wala tabia mbaya bali ni kupendeza na kuleta mvuto pia,familia hugubikwa na upendo furaha na amani ya kutosha mno,na watoto wa familia hizi huwa na uwezo mzuri pia wa kufikiri na kupambanua mambo. 

sasa tuangalie hali inakuwaje katika familia ya father/mother mara nyingi familia hizi ndio nyingi sana barani africa,na huwa mpangilio wa watoto mara nyingi huwa ni wengi sana tofauti na uwezo wa familia husika, wazazi katika familia hizi huwa ni maadui wa watoto,haswa wazazi wa kiume,baba anaposafiri katika familia hizi huwa ni sherehe kwa watoto na anapokuwa nyumbani huwa ni huzuni sana,vyakula huwa ni vya aina moja tu,na kunapopikwa vyakula ambavyo ni vizuri au vinavyoonekana kuwa vitamu kunakuwa na tukio maalumu labda sherehe,sikukuu au amekuja mgeni,watoto husoma shule zisizokuwa na elimu bora,watoto wadogo huenda kucheza mbali na nyumbani kwao na hawarudi mpaka watafutwe hurudi wakiwa wamechafuka sana na hupokelewa kwa vipigo vikali sana na kutukanwa matusi mazito kuliko umri wao,kunapopikwa chakula kizuri watoto huenda kufunua masufuria na vyungu vya kupikia na hapo huweza kudokoa chakula kabla ya kuandaliwa mezani,na mara nyingi watoto katika familia hizi huwa na upeo mdogo sana wa kufikiri

kuna baadhi ya waazi wengine wana maisha mazuri sana kama ya dady na mamy family,lakini kutokana na kuathiriwa na maisha ya father na mother walipokuwa wadogo na wao wanataka watoto wao wapitie maisha kama hayo,wakidhani kwamba ndio malezi bora kumbe huwa wanajidanganya wenyewe.
father na mother family.
wazazi watoto ni taifa la kesho na vijana ni taifa la leo tuwape afya bora,elimu bora na malezi kwani wao ni wajenzi wa taifa hili ni nguvu kazi na walezi wa kesho pia.
DADY AND MAMY FAMILY WAKIPATA CHAKULA CHA JIONI.
Kuna utofauti mkubwa pia hata wa kula vyakula,dady and mamy family wazazi na watoto hupata chakula kwenye meza ya pamoja kama unavyoona pichani lakini,kwenye familia ya father na mother hilo halipo watu hula chakula kila mmoja kivyake au kimakundi makundi,hali inayosababishwa na kukosekana kwa upendo au ufinyu wa maeneo ya kulia chakula,pia milo huwa ni zaidi ya mitatu,na kuna kuwa na vinywaji vya hapa na pale,matunda au vitu vya kutafuna baada ya mlo mmoja kuelekea mlo mwingine,wakati kwenye father na mother family,milo huwa mmoja, miwili au mi tatu tu pekee kulingana na kipato cha familia na kuna kuwa hakuna milo ya ziada kama ilivyo kwa dady and mamy family.


wazazi kumbukeni kujiandaa kabla ya kutengeneza familia ili kuweza kuwatengenezea watoto wenu maisha bora zaidi
  haya ni mawazo binafsi ya mwandishi na utafiti binafsi hayafungamani na upande wowote.




piga simu no 0656538476 kwa maoni na ushauri tu.

0 Response to "HII NDIO TOFAUTI KATI YA DADY/MAMY AND FATHER/MOTHER"

Chapisha Maoni